Dark
Light

Mwakinyo yuko tayari kupambana na mpinzani wake

Hassan Mwakinyo moja kati ya wanamasumbwi mashuhuri nchini Tanzania anatarajiwa kupanda ulingoni na mpinzani wake Mbiya Kanku toka DR Congo mnamo Januari 27, 2024.
January 22, 2024
by

Hassan Mwakinyo moja kati ya wanamasumbwi mashuhuri nchini Tanzania anatarajiwa kupanda ulingoni na mpinzani wake Mbiya Kanku toka DR Congo mnamo Januari 27, 2024.

Bondia Hassan Mwakinyo amesema amejiandaa kwa asilimia 98 hivyo kilichobaki ni kupima uzito pekee. Hassan ameongeza kwa kusema kuwa hakuna kitakachomfanya ashindwe kupata ubingwa kwani amekwishajiandaa kila idara na kilichobaki ni kuonyesha uweledi wake ulingoni.

Hata hivyo Mwakinyo amewatoa hofu mashabiki wake kwa kuwataka wajiandae tu kushuhudia jinsi atakavyoonyesha burudani ya kuvutia ya ngumi siku ya mpambano.

Hassan na mpinzani wake wanatarajiwa kukutana kwenye kinyang’anyiro cha mpambano wa ubingwa wa WBO Afrika utakaofanyika Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Mapambano mengine yatakayopigwa siku hiyo, ni mpambano kati ya Hussein Itaba na Juma Misumari wa Morogoro, Bakari H.Bakari na Seleman Hamad, Masoud Khatibu atazichapa na Yahaya Khamis, pasipo kusahau mwanadada Zulfa Iddi atakaevaana vikali na mpinzani wake Debora Mwenda.

Author

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Madagascar Military Takes Control After Rajoelina Ousted

 Madagascar’s political crisis deepened dramatically on Tuesday after the army

UN helicopter carrying ‘several’ foreigners captured by al Shabaab in Somalia

Al Shabaab militants captured a United Nations helicopter carrying two