Dark
Light

TANESCO: “Umeme Umekatika Baada Ya Hitilafu Gridi Ya Taifa”

TANESCO imeeleza baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Dodoma na Iringa Huduma imeanza kurejea huku Wataalamu wao wakiendelea na jitihada za marekebisho ili kurejesha Huduma hiyo Maeneo mengine
May 4, 2024
by

 Baada ya maeneo mengi Nchini kukosa Huduma ya Umeme kuanzia usiku wa kuamkia leo Mei 4, 2024, Shirika la Umeme Tanzania [TANESCO] limesema hali hiyo imesababishwa na hitilafu kwenye Mfumo wa Gridi ya Taifa iliyotokea majira ya Saa 8:40 Usiku

TANESCO imeeleza baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Dodoma na Iringa Huduma imeanza kurejea huku Wataalamu wao wakiendelea na jitihada za marekebisho ili kurejesha Huduma hiyo Maeneo mengine

Soma Zaidi:TANESCO Gets New Board of Directors to Address Country’s Power Crisis

Nukuu ya Taarifa kwa Uma iliyo tolewa na shirika hilo ni ” Shirika la Umeme Tanzania [TANESCO] linawataarifu wake kuwa hitilafu iliyojitokeza katika mfumo wa gridi ya taifa imefanywa kazi na wataalamu wetu

Mpaka sasa huduma ya umeme imerejeshwa kupitia vituo vyetu vya kupokea, kupoozea na kusambaza umeme Nchini na tayari maeneo mengi yanapata huduma

Shirika linawashukuru wateja wake wote kwa uvumilivu katika kipindi chote ambacho huduma hii ilikosekana”

Awali kabla ya taarifa hiyo, Shirika hilo lilitoa taarifa ya kukosekana kwa umeme katika baadhi ya maeneo, huku ikithibisha kuwepo kwa jitihada ya wataalamu kufanyia kazi hitilafu hiyo na kuhakikisha umeme unarudi katika maeneo yote.

6 Comments

  1. I do accept as true with all of the concepts you’ve introduced for your post. They’re very convincing and will definitely work. Still, the posts are very quick for newbies. May just you please lengthen them a little from next time? Thanks for the post.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Behind Global Politics: Power, Dynasties, and the Illusion of Change

Politics, at its core, should represent the will of the

Putin Unveils Medal for Great Patriotic War

Russian President Vladimir Putin, has signed a decree to establish