Dark
Light

Tanzania Na Urusi Kupaisha Utalii

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan kujadili masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi ikiwemo utalii.
March 26, 2024
by

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan kujadili masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi ikiwemo utalii.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Makamba na Balozi Avetisyan wamejadili umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta ya utalii ikiwemo kuendelea kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini kutoka nchi hiyo.

Baadhi ya mambo yanayotazamiwa ni pamoja na kusaini Mkataba wa Ushirikiano katika Masuala ya Anga (BASA).

Mhe Waziri Makamba alitumia nafasi hiyo pia kutoa salamu za pole kwa Urusi kufuatia vifo vya watu zaidi ya 130 vilivyotokana na shumbilio la kigaidi lililotokea jijini Moscow hivi karibuni.

Author

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Bodi Ya Maziwa Yapewa Maagizo Na Serikali

Serikali imeiagiza Bodi ya Maziwa Nchini kujadili kwa haraka na

Tragic Truck Accident in Ethiopia Claims 71 Lives

A devastating truck accident in southern Ethiopia has left at