Dark
Light

Aliyefariki Miaka Sita Iliyopita Aonekana Akichunga Ng’ombe

Familia ya Magesa pia ilishangaa na kusikitika kwa taarifa za urejeo wake. Mwanafamilia, Emanuel Rutubwi, alisema kuwa wallikubali kifo chake na kumzika kwa heshima, lakini sasa wanashangaa kumwona akiwa hai.
May 16, 2024
by

Wakazi wa kijiji cha Nyakatende, halmashauri ya wilaya ya Musoma mkoani Mara, walipoendelea na shughuli zao za kila siku ili kupambania familia zao kuwa na uchumi bora, walipokea habari inayoshangaza na kuibua taharuki kubwa. Kijana aliyeitwa Magesa Lucas, ambaye kwa miaka sita iliyopita aliaminiwa kuwa amefariki dunia na maiti yake kuzikwa kijijini Nyambui mkoani Mara, alirudi ghafla katika kijiji chao.

Mkazi wa Nyakatende, Juma Magesa, ambaye alikuwa shuhuda wa mazishi ya awali ya Magesa, alisema kuwa walimzika miaka sita iliyopita. Lakini mwingine mkazi, Pendo Keya, alielezea kuwa walishindwa kuelewa ni nani aliyekuwa amezikwa wakati huo.

Soma Pia:Hidaya Asababisha Vifo 5 , Uharibifu Mkubwa Nchini Tanzania

Familia ya Magesa pia ilishangaa na kusikitika kwa taarifa za urejeo wake. Mwanafamilia, Emanuel Rutubwi, alisema kuwa wallikubali kifo chake na kumzika kwa heshima, lakini sasa wanashangaa kumwona akiwa hai.

Uongozi wa kijiji cha Nyakatende ulieleza kuwa walipopata taarifa za kurudi kwake, walitembea na kufuatilia suala hili kwa undani. Kijana Magesa mwenyewe alipoulizwa, alieleza shughuli alizokuwa akifanya katika miaka sita iliyopita, akiondoa taharuki miongoni mwa wakazi.

Hata hivyo, suala hili limezua maswali mengi, na mamlaka husika zimethibitisha kufanya uchunguzi kina. Mwenyekiti wa serikali ya kijiji, Atanas Rusaro Maganga, alisema kuwa watoa taarifa kwa umma mara uchunguzi utakapokamilika.

Tukio hili limeacha wakazi wa Nyakatende na maswali mengi yasiyojibiwa, na kusababisha taharuki na mshtuko katika kijiji chao. Maafisa husika wameahidi kufanya uchunguzi kamili ili kuleta mwangaza juu ya tukio hili la kushangaza.

1 Comment

  1. Can I just say what a relief to find someone who actually knows what theyre talking about on the internet. You definitely know how to bring an issue to light and make it important. More people need to read this and understand this side of the story. I cant believe youre not more popular because you definitely have the gift.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

BoT Purchases Over Sh400 Billion Worth of Gold

The Bank of Tanzania (BoT) has bought more than Sh400

Deputy Minister Londo Bids For Economic Opportunities in Russia

Deputy Minister of Foreign Affairs and East African Cooperation dealing