Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Februari 12, 2024 amekutana na Papa Francis jijini Vatican na kufanya naye mazungumzo.
Viongozi hao wamejadiliana masuala mbalimbali, ikiwemo mchango wa Kanisa Katoliki katika uboreshaji wa huduma mbalimbali za kijamii hususani elimu, afya na misaada ya kijamii pamoja na ushirikiano wa kimataifa wa pande zote mbili kujitolea kukuza amani dunia.
Wakati huo huo, Rais Samia amekutana na Katibu Mkuu wa Vatican, Kadinali Pietro Parolin na viongozi wengine akiwemo Paul Richard Gallagher anayeshughulikia uhusiano wa Vatican na mataifa mbalimbali duniani.
Sambamba na hilo Baba mtakatifu Francis amemteua Padre Wilbroad Kibozi wa jimbo kuu Katoliki Dodoma kuwa Askofu msaidizi wa jimbo hilo kuanzia leo,kabla ya uteuzi huo Askofu Kibozi alikuwa makamu Gambera, mlezi na mwalimu wa Seminari kuu ya kitaifa ya familia takatifu-Mwendakulima iliyopo jimboni kahama
These are actually great ideas in concerning blogging.
You have touched some pleasant factors here. Any way keep up wrinting.
I think the admin of this web site is actually working hard
for his web page, because here every information is quality based
data.