Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango kwa niaba ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameongoza Viongozi na Waombolezaji wengine kwenye shughuli za kumuaga Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam leo February 13,2024.
Wengine walioshiriki kumuaga Lowassa ambaye alifariki juzi February 10,2023 JKCI, Dare salaaam ni pamoja na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi na Mkewe Mariam Mwinyi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Marais Wastaafu Dkt. Jakaya Kikwete na Dkt. Shein, Mawaziri Wakuu Wastaafu Fredrick Sumaye na Joseph Warioba.
Wengine ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso, Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, Katibu Mkuu wa UWT Jokate Mwegelo, RC wa Dar es salaam Albert Chalamila na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo.(swipe kuona picha nyingine)
Additional Source: Millardayo