Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Samia Aonesha Masikitiko kwa Kifo cha Mtoto Mwenye Ualbino

June 18, 2024
by

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha masikitiko makubwa kutokana na kifo cha kusikitisha cha mtoto mwenye ualbino, Asimwe Novath.

Mnamo tarehe 17 Juni 2024, mwili wa Asimwe, mwenye umri wa miaka miwili na nusu, ulipatikana ukiwa umefungwa kwenye mfuko wa sandarusi huku baadhi ya viungo vyake vikiwa havipo

Asimwe, mkazi wa Kitongoji cha Mbale, Kijiji cha Bulamula, kata ya Kamachumu, wilaya ya Muleba mkoani Kagera, alitekwa nyara mnamo Mei 30, 2024. Mama yake, Judith Richard, alieleza kuwa watekaji walijifanya wanahitaji msaada wa haraka baada ya kuumwa na nyoka. Walipofungua mlango kuwasaidia, walimnyonga na kumchukua mtoto wake

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Yusuph Daniel, alithibitisha kuwa watu watatu, akiwemo baba wa mtoto huyo, wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hili. Aliendelea kusema kuwa juhudi za kumsaka mtoto huyo zilikuwa zinaendelea kwa nguvu zote

SomaZaidi;Polisi Afrika Mashariki Waungana Waadhimisha Mauaji Ya Kimbari

Tukio hili limevutia hisia kali kutoka kwa mashirika mbalimbali, ikiwemo Tanzania Albino Society (TAS). Mwenyekiti wa TAS, Godson Mollel, alilaani vikali tukio hili na kusema kuwa ni aibu kwa taifa linalojigamba kuheshimu utu wa binadamu kuwa na raia wake wenye ualbino wakiishi kwa hofu. Alisisitiza umuhimu wa serikali kuchukua hatua kali na za haraka kukomesha vitendo vya kinyama kama hivi

Dr. Abel Nyamahanga, Mkuu wa Wilaya ya Muleba, ameelekeza viongozi wa vijiji kufanya sensa ili kubaini na kulinda watu wenye ualbino katika wilaya hiyo. Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya usalama ili kuhakikisha kuwa wahalifu wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria

Kwa muda mrefu, watu wenye ualbino wamekuwa wakikabiliwa na manyanyaso na mauaji kutokana na imani potofu za kishirikina. Tukio hili linaonyesha kuwa tatizo hili bado lipo, licha ya juhudi za serikali na mashirika mbalimbali za kupambana na unyanyasaji huu.

Wakati jitihada za kuwasaka wahusika zikiendelea, wananchi na viongozi wanatoa wito kwa serikali kuongeza juhudi za kulinda maisha ya watu wenye ualbino na kuhakikisha kuwa haki inatendeka kwa waathirika wa vitendo vya kikatili kama hivi.

Author

2 Comments

  1. Hello there! Quick question that’s totally off topic. Do you know how to make your site mobile friendly? My web site looks weird when browsing from my iphone. I’m trying to find a template or plugin that might be able to fix this issue. If you have any recommendations, please share. Thanks!

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Trump’s ICC Sanctions Hinder Tribunal’s Operations, Staff Say

ICC staff members report that sanctions imposed by the Trump

Burkina Faso Bans Homosexual Unions

Burkina Faso has announced a ban on homosexual acts, making