Breaking News
Breaking News
Dark
Light

“Simba Imeingia Mtegoni,Watu Waongeza Chumvi”-Ahmed Ally

"Timu yetu inapitia kipindi kigumu Lakini ni tofauti na inavyozungumzwa yaani wanaongeza chumvi
April 11, 2024
by

Meneja wa habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba ,Ahmed Ally ameandika ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram kuhusu wakati mgumu wanaokutana nao klabu hiyo kutokana na kuongezwa chumvi kwa watu.

Ahmed Ally ameandika maneno hayo baada ya kutolewa na timu ya Mashujaa katika mashindano ya CRDB Confederation Cup ikiwa ni muendelezo wa matokeo mabaya baada ya kutolewa Ligi Ya Mabingwa Afrika hatua ya robo fainali

“Timu yetu inapitia kipindi kigumu Lakini ni tofauti na inavyozungumzwa yaani wanaongeza chumvi

Huu ni mpango wa makusudi unaoratibiwa na wasiotutakia mema, Bahati mbaya ni kwamba Wana Simba tumeingia kwenye mtego wa kujidharau na kujitukana

Tukiwa na Simba Bora sana tuliwahi kutolewa hatua ya awali ya ligi ya Mabingwa Afrika na UD Songo, Tukiwa na Simba Bora tuliwahi kutolewa na Green Warrios kwenye Kombe la Shirikisho

Haya mi Maisha ya kawaida kwenye mpira wa miguu

Kila timu ya mpira hupitia nyakati kama hizi, Ila tukipitia Simba basi huonekana ni kitu cha ajabu inawezekana tunahukumiwa na ukubwa wetu

Read>> Simba all set for showdown with Mashujaa in Kigoma today

https://mediawireexpress.co.tz/simba-all-set-for-showdown-with-mashujaa-in-kigoma-today/

Leo watakuambia wachezaji wabovu, kesho Muwekezaji tatizo, kesho kutwa Viongozi hawafai

Hivi tungekua na matatizo yote hayo si tungekua tumeshuka daraja?

Wengine wanaibuka kukashifu viongozi na kudhihaki wachezaji wakiamini huko ndio kuipenda Simba au wao ndio wenye uchungu sana na Simba

Wakati Nyuma Mwiko wako dhofli hali waliibuka na kauli ya kusema tumeipenda wenyewe acha ituue, Hii ilikua kauli ya kishujaa sana na waliamua kufa na timu yao

Read>> Embrace constructive criticism – Mangungu tells Simba

https://mediawireexpress.co.tz/?s=simba
Kwa sasa hatuna budi kusimama na timu yetu ili mambo yasiharibike zaidi, hatuwezi kubadili yaliyopita ila tunaweza kutengeneza yajayo

Tulichobakiwa nacho ni Ligi Kuu ya NBC, Kwa pamoja tuwekeze nguvu kwenye kombe hili

Tuache kulaumiana, tuhamishie machungu yetu na tuelekeze hasira zetu kwenye ligi

Pengo ni alama 4 tukisimama sawa sawa kwa umoja wetu tunaliondoa

Hii inaanza na mechi ya Tarehe 13 dhidi ya Ihefu, na baada ya hapo mechi ya tarehe 20, tukichukua alama 6 kwenye mechi hizi tutakua pazuri sana” Ahmed Ally

Author

4 Comments

  1. Thank you for your sharing. I am worried that I lack creative ideas. It is your article that makes me full of hope. Thank you. But, I have a question, can you help me?

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Another casualty recorded amid chieftaincy dispute at Nkwanta

Another person has been shot dead at Nkwanta in the

Dozens nabbed for hiking sugar prices

A total of 84 retail traders have been arrested for