Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Takwimu 2014-2023 Watumiaji wa Bangi na Mirungi

Katika mwaka 2023 kiasi cha tani 1,757.56 za dawa za kulevya aina ya bangi kilikamatwa kikihusisha watuhumiwa 8,803 kati yao wanaume 8,180 na wanawake 623.
May 17, 2024
by

Operesheni na ukamataji uliofanywa na Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini ilifanikiwa kukamata dawa za kulevya za mashambani aina ya bangi na mirungi pamoja na dawa za viwandani aina ya heroin, cocaine, methamphetamine na dawa tiba zenye asili ya kulevya kama ilivyoainishwa

Katika mwaka 2023 kiasi cha tani 1,757.56 za dawa za kulevya aina ya bangi kilikamatwa kikihusisha watuhumiwa 8,803 kati yao wanaume 8,180 na wanawake 623. Aidha, katika kipindi hiki kumeibuka uingizaji na matumizi ya bangi mpya inayoitwa “skanka” ambayo inadhaniwa kuwa inazalishwa nchi za kusini mwa Afrika. Skanka ni mchanganyiko wa aina mbili za bangi, Cannabis sativa na Cannabis indica, ikiwa na kiasi kikubwa cha THC hivyo kuwa na athari kubwa zaidi kwa watumiaji.

Mirungi ni dawa ya kulevya ya mashambani ambayo pia imeendelea kuwa tatizo kwa mwaka 2023. Mwaka 2023, jumla ya tani 202.74 za dawa hii zilikamatwa zikihusisha watuhumiwa 1,179 kati yao wanaume 996 na wanawake 183.

Soma: Afungwa Miaka 60 Jela:kosa Ukatili Wa Watoto

Kiasi cha bangi tani 1,757.56 kilichokamatwa mwaka 2023 ni zaidi ya mara tano ya kiasi kilichokamatwa kwa miaka tisa iliyopita kuanzia mwaka 2014 hadi 2022 ambacho kilikuwa tani 326.09. Aidha, kiasi cha mirungi tani 202.74 kilichokamatwa kwa mwaka mmoja wa 2023, kinazidi kiasi cha mirungi kilichokamatwa kwa miaka tisa iliyopita (kuanzia mwaka 2014 hadi 2022) ambacho kilikuwa tani 177.78. Mafanikio haya yametokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ikiwemo uwezeshaji, utashi wa kisiasa na ushiriki wa wananchi katika kutoa taarifa.

Author

9 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Putin Agrees to Pause Strikes After Trump Call

Russian President Vladimir Putin has ordered a temporary halt to

New Report ranks TTCL last in service quality among Tz Networks

A new report by the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA)