Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Wahasisi wa Maandaano Kariakoo Matatani

"Wafanyabiashara watakaokaidi agizo ambalo lilisema kuwa mshale wa jicho utakuwa haki yake".
June 23, 2024
by

Jeshi la Polisi Nchini limesema kuwa tangu Juni 22, 2024 kupitia baadhi ya vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii kulionekana tangazo linalosambazwa lenye kichwa cha habari kilichosomeka “KUFUNGA BIASHARA ZETU”.

Akitoa taarifa hiyo leo jijini Arusha Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini Naibu kamishna wa Polisi DCP David Misime amesema tangazo hilo lina ujumbe unaosema “Wafanyabiashara wote wa viunga vya Kariakoo mnatakiwa kufunga biashara zenu zote ikiwemo maduka yenu, ofisi zetu na chochote unachokifanya kuanzia Jumatatu ya Juni 24, 2024 bila ukomo hadi pale changamoto zetu zote za kibiashara zitakapoweza kutatuliwa”.

DCP Misime amesema kuwa Mbali na tangazo hilo kutokujulikana limetolewa na nani, amebainisha kuwa limeenda mbali zaidi hadi kukiuka sheria za nchi kwa kutangaza vitisho kuwa; “Wafanyabiashara watakaokaidi agizo ambalo lilisema kuwa mshale wa jicho utakuwa haki yake”.

Soma:Mbowe: Tathmini Ya Maandamano Kwa Mikoa 13

Ameendeleaa kusema kuwa Uongozi wa Umoja wa Wafanyabiashara wa soko la Kariakoo wameeleza kuwa tangazo hilo halijatoka kwao na hata uongozi wao ngazi ya Taifa hawajathibitisha tangazo hilo kutoka kwao.

Vile vile amesema Jeshi la Polisi nchini linapenda kuwahakikishia wafanyabiashara na wananchi wote kwa ujumla ambao wanafanya shughuli zao za biashara na kupata mahitaji katika soko hilo kuwa ulinzi utaimarishwa ipasavyo katika maeneo yote huku likabainisha kuwa wakati walio kula njama, kuandaa na kusambaza tangazo hilo wakitafutwa.

Jeshi la Polisi Nchini limewaomba wananchi kuendelea na shughuli zao kama kawaida bila hofu.

Pia Msemaji wa Jeshi hilo amesema Jeshi la Polisi linatoa wito kwa mtu yeyote mwenye changamoto zenye kuhitaji utatuzi afuate utaratibu wa kuzifikisha kwenye mamkaka husika ili zifanyiwe kazi na sio kuvunja sheria kwa kutoa vitisho na kulazimisha wengine kutekeleza/kufanya yale ambayo hawakubaliani na waliotoa tangazo hilo.

Author

9 Comments

  1. F*ckin¦ awesome things here. I¦m very glad to look your post. Thanks a lot and i am taking a look forward to contact you. Will you kindly drop me a mail?

  2. I’m not sure where you’re getting your info, but good topic. I needs to spend some time learning much more or understanding more. Thanks for wonderful info I was looking for this information for my mission.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Tanzania and India Strengthen Energy Cooperation

Tanzania’s Deputy Prime Minister and Minister for Energy, Dr. Doto

Mmoja afariki, watatu wajeruhiwa ajali ya gari Njombe

Dereva wa gari la mizigo Adriano Samweli (40) mwenyeji wa