Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Rais Dk.Mwnyi Aifariji Familia ya Lowassa

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema amewahi kufanya kazi na Hayati Edward Lowassa kwa vipindi tofauti katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya awamu ya tatu na awamu ya nne.
February 13, 2024
by

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema amewahi kufanya kazi na Hayati Edward Lowassa kwa vipindi tofauti katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya awamu ya tatu na awamu ya nne.

Amesema taarifa ya msiba huu ameipokea kwa masikitiko makubwa, pia anatoa pole kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wananchi wote kwa ujumla.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipofika nyumbani kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Hayati Edward Lowassa, akiwa na Mama Mariam Mwinyi, kwa lengo la kuwafariji wanafamilia wa marehemu akiwemo Mama Regina Lowassa, Masaki, Jijini Dar es Salaam, tarehe 12 Februari 2024.

Credit:Ikulu habari

Author

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Tanga Police Arrest Suspect in Tragic Arson Attack

Police in Tanga have arrested Mwita Yoba Chacha, the man

Simbachawene Encourages Leaders to Trust Capable Employees

The Minister for Public Service Management and Good Governance, George