Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Atuhumiwa Kumuua Mke Wake Kisha Kumzika Chumbani

Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamshikilia Mohamed Omary Salahange (37) mkazi wa Rudewa Gongoni wilayani Kilosa kwa tuhuma za kumuua kisha kumzika kwenye chumba walichokuwa wakiishi, mke wake Beatrice Talius Ngongolwa.
March 22, 2024
by

Jeshi la polisi mkoani Morogoro linamshikilia Mohamed Omary Salahange (37) mkazi wa Rudewa Gongoni wilayani Kilosa kwa tuhuma za kumuua kisha kumzika kwenye chumba walichokuwa wakiishi, mke wake Beatrice Talius Ngongolwa.

Kamanda wa polisi mkoani humo, SACP Alex Mkama amesema jeshi hilo lilipokea taarifa za siri kuhusu mauaji hayo mnamo Machi 21 zilizoeleza kuwa mtuhumiwa wa mauaji hayo alitenda kosa hilo na kuhama kwenye nyumba aliyokuwa akiishi na mkewe.

Jeshi la polisi limeongeza kuwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa mtuhumiwa alikiri kufanya mauaji hayo na aliwapeleka maafisa wa polisi kwenye eneo la tukio ambako jeshi la polisi kwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali pamoja na kamati ya usalama wilaya ya Kilosa waliufukua mwili wa mwanamke kwaajili ya uchunguzi zaidi.

Jeshi hilo linaendelea na hatua zaidi za uchunguzi wa kimaabara ili kukamilisha upelelezi kwa ajili ya hatua za kisheria.

 

Source: azammedia

Author

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

New Testing for Graduate Teachers Announced

Starting next year, graduate teachers in Tanzania will face stringent

Indian Billonnaire Adani expands business interest in Dar Port

Indian firm, Adani International Port Holdings Pte Limited (AIPH), owned