Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Ummy Akerwa kadi za kliniki kuuzwa

Ummy alibainisha hayo jana jijini hapa alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya ugawaji wa vitabu vya kufuatilia maendeleo ya mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano, iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Dodoma.
May 11, 2024
by

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, amesema anakerwa na tabia iliyozuka katika hospitali na vituo vya afya kuuza kadi za kliniki kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kinyume cha Sera ya Afya.

Kutokana na hali hiyo amepiga marufuku tabia ya watumishi katika kada hiyo muhimu kuuza kadi hizo.

Ummy alibainisha hayo jana jijini hapa alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya ugawaji wa vitabu vya kufuatilia maendeleo ya mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano, iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Dodoma.

Also Read:Serikali Yadhamiria Kuboresha Huduma za Ukunga

“Kuna jambo ambalo linanikera sana. Hivi sasa kadi za kliniki kwa ajili ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano hazipatikani. Wanasema hazipo lakini kadi zinauzwa na sera inasema kadi ni bure. Nasisitiza Katibu Mkuu Wizara ya Afya sitaki kusikia mjamzito anauziwa kadi ya kliniki.

“Mjipange leo hapa tunagawa kadi milioni 1.2 lakini kwa mwaka makadirio ya mahitaji ya kadi ni milioni 1.4. kati ya bidhaa ambazo sitaki kusikia haipatikani ni kadi hizi za kliniki kama nilivyoelekeza kwenye upatikanaji wa damu hata kama bajeti itatoka kidogo mhakikishe kadi zinakuwapo za kutosha. Moja ya vitu vya kipaumbele ni kadi za wajawazito na watoto chini ya miaka mitano,” alisisitiza.

Pia alisema waganga wakuu lazima wafuatailie usambazji wa kadi pamoja na makisio yao ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kwa mwaka.

Akizungumzia kuhusu hali ya wajawazito kuhudhuria kliniki, alisema kwa hivi sasa asilimia 80 ya wanaenda kliniki angalau mara nne katika kipindi chao cha ujauzito.

“Lakini bado hatufanyi vizuri kwa kuwa mahudhurio ya kwanza ni asilimia 41 tu ndiyo wanahudhuria chini ya wiki 12 au miezi mitatu tangu kupata ujauzito. Twendeni tukahamasishe kinamama kwenda kliniki mapema.

“Ukiwahi kuna changamoto ya kuzaa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi unazipunguza, hivyo kama mama mwezi wa kwanza hujaona wageni (hedhi), wa pili hujaona wageni, basi nenda kliniki utafanyiwa vipimo na kama mjamzito utaanza kliniki mapema,” alisema.

Kadhalika, alisema upatikanaji wa vitabu vya kliniki kwa ajili ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano utatumika kuwapima utendaji wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya pamoja na yule wa Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

“Naelekeza mjipange vizuri kuhakikisha vitabu hivi vinapatikana mapema kwenye maeneo yote. Hilo ndilo tutampima Katibu Mkuu Afya na TAMISEMI. Hii kero tunaimudu kuitatua, hatupaswi kuona upungufu wa vitabu vya kliniki nchini,” alisema.

Author

4 Comments

  1. Jangan sampai tergiur dengan tawaran hadiah besar kalau
    link-nya mencurigakan. Bisa aja itu trik buat dapatin data pribadi kamu.
    Lebih baik abaikan kalau nggak jelas!.

  2. Banyak yang mengeluh setelah menggunakan situs ini. Mereka tertarik
    karena promosi besar-besaran, tapi setelah beberapa waktu,
    akun mereka diblokir tanpa alasan yang jelas. Jika ini benar-benar situs terpercaya, seharusnya mereka memiliki layanan pelanggan yang
    bisa membantu pengguna dengan transparan!

  3. Good – I should definitely pronounce, impressed with your website. I had no trouble navigating through all tabs and related information ended up being truly simple to do to access. I recently found what I hoped for before you know it in the least. Quite unusual. Is likely to appreciate it for those who add forums or anything, website theme . a tones way for your customer to communicate. Nice task..

  4. Magnificent goods from you, man. I’ve take into account your stuff previous to and you’re simply too fantastic.
    I really like what you’ve acquired here,certainly like
    what you are stating and the best way during which you assert it.

    You’re making it entertaining and you continue to care for to keep it smart.

    I can not wait to read much more from you. This is actually a
    tremendous website.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Putin Skips Turkey Peace Talks, Delegation Sent

Russian President Vladimir Putin has opted not to attend upcoming

Three Arrested for Counterfeit Currency Operation in Mara

The Mara Regional Police have arrested three individuals who were