Dark
Light

Vyakula vilivyoletwa na Marekani ni salama-TBS

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limesema Mchele, Mafuta ya kupikia ya Alizeti na Maharage ambavyo vimeongezwa Virutubisho vilivyotolewa na Wizara ya Kilimo ya Marekani kwa ushirikiano na Taasisi ya Jumuiya za Kimataifa (Global Communities) kwa baadhi ya Shule za Dodoma, vyote ni salama kwa Walaji
March 18, 2024
by

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limesema Mchele, Mafuta ya kupikia ya Alizeti na Maharage ambavyo vimeongezwa Virutubisho vilivyotolewa na Wizara ya Kilimo ya Marekani kwa ushirikiano na Taasisi ya Jumuiya za Kimataifa (Global Communities) kwa baadhi ya Shule za Dodoma, vyote ni salama kwa Walaji

Taarifa hiyo ya TBS imesema taratibu za uingizwaji wa chakula Nchini zilifuatwa ikiwemo ukaguzi na uchunguzi wa Kimaabara

Meneja Uhusiano na Masoko wa TBS, Gladness Kaseka amesema “Utaratibu wa kuongeza virutubisho kwenye chakula (food fortification) unakubalika kitaalamu na hufanyika kwa lengo la kuboresha hali ya lishe kwa walaji.”

Aidha shirk hilo limesisitiza litaendelea kuhakikisha chakula kinachoingia nchini kinakidhi vigezo vya usalama na bora kwa mujibu wa matakwa ya viwango ili kuendelea kulinda afya ya walaji.

Sambamba na hilo Siku chache zilizopita Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alisema Taasisi hiyo ya Marekani inunue vyakula kutoka kwa Wakulima wa Tanzania na Virutubisho viwekwe huku Watanzania wakishuhudia.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Government Launches Initiative to Expand Indigenous Forests

The Tanzanian government has announced an initiative to increase indigenous

Nape Urges Media to Amplify 4Rs Philosophy

Minister for Information, Communication and Information Technology, Mr Nape Nnauye,