Dark
Light

Mmoja afariki, watatu wajeruhiwa ajali ya gari Njombe

Mashuhuda wameeleza namna walivyoshirikiana kuwaokoa watu waliokuwemo kwenye gari hilo baada ya ajali kutokea, na kulazimika kuchimba shimo ili kuweza kuutoa mwili wa marehemu.
June 9, 2024
by

Dereva wa gari la mizigo Adriano Samweli (40) mwenyeji wa Kigoma, amefariki dunia katika ajali iliyotokea Kijiji cha Igumbilo, Kata ya Lupila wilayani Makete mkoani Njombe baada ya kushindwa kulimudu gari hilo na kisha kutumbukia korongoni.

Ajali hiyo imetokea usiku kuamkia jana Juni 8, 2024 katika Mtaa wa Ihagala, Kitongoji cha Kisekelewe ambapo gari hilo lilibeba viazi na kulikuwa na watu wanne.

Utingo wa gari hilo, Riziki Shaban ameeleza namna alivyonusurika katika ajali hiyo kwa kusema ni kwa neema za Mungu kwani lilipoanza kubiringika yeye lilimtupa nje na kuendelea kuporomokea korongoni.

Soma:Dereva Shabiby Atuhumiwa Kusababisha Ajali majeruhi 22

Mashuhuda wameeleza namna walivyoshirikiana kuwaokoa watu waliokuwemo kwenye gari hilo baada ya ajali kutokea, na kulazimika kuchimba shimo ili kuweza kuutoa mwili wa marehemu.

Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Lupila, Dk Isack Lulindi akizungumza ofisini kwake amesema ni kweli walipokea majeruhi watatu ambao wamewatibu na tayari wameruhusiwa, pia wamepokea mwili wa mtu mmoja akiwa amefariki dunia na umehifadhiwa kituoni hapo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Mahamoud Banga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akitaja kuwa chanzo ni dereva kushindwa kulimudu gari hilo na kutumbukia korongoni.

Kamanda Banga ametoa wito kwa madereva wageni na jiografia ya Mkoa wa Njombe kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kuwatumia wenyeji wanapokuja kuchukua mizigo ili kuepusha matukio ya ajali.

 

Source: Mwanachi Digital

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Mpina Afungiwa Vikao 15 Bungeni

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeidhinisha adhabu ya

Lissu Takes Over Leadership at Tanzania Centre for Democracy

Tundu Lissu, the newly elected chairman of Chadema, has officially