Dark
Light

EAPP Zakubaliana Kuipa Msukumo Miradi Ya Umeme

Baraza la Mawaziri wanaohusika na mfumo wa pamoja wa umeme kwa nchi za Mashariki mwa Afrika (EAPP Council of Ministers-COM) limekubaliana kwa pamoja kuwa na usimamizi madhubuti wa miradi mbalimbali ya umeme katika nchi wanachama, ili iweze kukamilika kwa wakati na kuwapatia wananchi nishati ya kutosha.
February 28, 2024
by

Baraza la Mawaziri wanaohusika na mfumo wa pamoja wa umeme kwa nchi za Mashariki mwa Afrika (EAPP Council of Ministers-COM) limekubaliana kwa pamoja kuwa na usimamizi madhubuti wa miradi mbalimbali ya umeme katika nchi wanachama, ili iweze kukamilika kwa wakati na kuwapatia wananchi nishati ya kutosha.

Kukamilika kwa miradi kutoka vyanzo mbalimbali vya umeme, kutawezesha nchi hizo kusaidiana pale nchi mojawapo inapokuwa na upungufu wa umeme huku msisitizo ukiwekwa kwenye miradi ya usafirishaji umeme.(Transmission lines).

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko tarehe 27 Februari 2024 katika Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wanaohusika na mfumo wa pamoja wa umeme kwa nchi za Mashariki mwa Afrika (EAPP Council of Ministers-COM) ambao unafanyika kwa siku mbili jijini Nairobi, Kenya.

“ Baraza hili ni muhimu katika kuhakikisha nchi za Afrika zinaungana kwa ajili ya kuendeleza rasilimali za umeme zilizopo pamoja na kupata umeme wa uhakika kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, na katika Mkutano huu kila nchi imeonesha utayari kufanya biashara ya umeme pale kunapokuwa na umeme wa ziada.” Amesema Dkt. Biteko

Ameeleza kuwa kuna idadi kubwa ya watu katika nchi wanachama wa EAPP, hivyo inahitajika nishati zaidi kwa ajili ya maendeleo ya watu na viwanda na ndio maana kila nchi imejikita katika kuendeleza vyanzo mbalimbali vya umeme ajili ya kujipatia nishati ya uhakika.

Amesema kuwa, Tanzania itakuwa sehemu ya soko la umeme pale nchi jirani zitakapohitaji nishati hiyo, na hii ni baada ya kuwashwa kwa mashine zote Tisa katika Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere ambalo litazalisha megawati 2,115 ambazo zinatoa uhakika wa kutosheleza mahitaji ya ndani.

 

Ameongeza kuwa, kuna upembuzi yakinifu unafanyika chini ya Benki ya Dunia (WB) kwa ajili ya kujenga mradi mkubwa wa usafirishaji umeme wa msongo wa Kilovoti 400 kutoka Tanzania hadi Uganda kutokea Shinyanga, ambao utasafirisha umeme mwingi zaidi kwa baadhi ya mikoa kama vile Kagera na pia kuwezesha nchi hizo kufanya biashara ya umeme.

34 Comments

  1. Sekarang banyak banget penipuan online yang mirip banget sama
    situs terkenal. Jangan sampai ketipu ya! Cek
    URL dan pastikan protokol keamanannya aktif sebelum kasih data.

  2. I was curious if you ever considered changing the page layout of your website? Its very well written; I love what youve got to say. But maybe you could a little more in the way of content so people could connect with it better. Youve got an awful lot of text for only having one or two pictures. Maybe you could space it out better?

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Areas Designated For Small-Scale Miners In Songwe

Deputy Minister of Minerals, Dr. Steven Kiruswa, met with small-scale

Russia, US Urge Immediate UN Action on Syrian Violence

 Russia and the United States have come together to request