Breaking News
Breaking News
Dark
Light

Nchi 4 Kujifunza Uchimbaji Madini Tanzania

Ukuaji na Maendeleo ya Sekta ya Madini Tanzania umezivutia nchi nne za Kenya , Uganda , Zambia na Msumbiji kuja kujifunza Usimamizi wa Rasilimali madini na kubadilishana uzoefu kuhusu uchimbaji endelevu.
June 29, 2024
by

Ukuaji na Maendeleo ya Sekta ya Madini Tanzania umezivutia nchi nne za Kenya , Uganda , Zambia na Msumbiji kuja kujifunza Usimamizi wa Rasilimali madini na kubadilishana uzoefu kuhusu uchimbaji endelevu.

Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu wizara ya madini, Msafiri Mbibo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la _Africa Resilience Dialogue_ (ARD) lililofanyika Jijini Dodoma.

Akielezea kuhusu ukuaji wa Sekta ya Madini Tanzania Mbibo alisema kuwa, kufikia 2023 sekta ilikuwa kwa asilimia 11.3 kutoka asilimia 10.8 kwa mwaka 2022.

Mbibo alifafanua kuwa, sekta ya madini ni miongoni mwa sekta za uziduaji ambazo kama hazitafanyika kwa uangalifu zinaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira na hivyo kuathiri afya na usalama wa wananchi wa maeneo husika.

Soma:Serikali yapiga marufuku wageni kununua madini ‘gesti’

Kuhusu usimamizi wa sekta Mbibo alieleza kuwa, Wizara ya madini imeendelea kusimamia ushiriki wa wadau mbalimbali vikiwemo Vyama vya Wachimbaji wadogo kama vile TwiMMI na TAWOMA ili kuhakikisha kwamba wanawake wananufaika ipasavyo katika mnyororo mzima wa sekta ya madini.

Sambamba na ushiriki wa kisekta kimataifa , Mbibo aliongeza kuwa Tanzania ni nchi mwanachama wa Jumuhiya ya _Extractive Industry Transparency Initiative (_ EITI) ambapo mikataba na mapato yote ya sekta za Uziduaji ikiwemo sekta ya madini huwekwa wazi kwa wananchi na nchi ambazo ni jumuhiyo wanachama.

Naye, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo wa Madini (TWiMMI) , Paulina Ninje alipongeza jinsi sekta ya madini inavyotoa ushirikiano mkubwa kwa vyama vya wanawake wanaojishughulisha na uchimbaji madini nchini.

Ninje aliongeza kuwa kwasasa chama cha TwiMMI kina miradi mbalimbali na kimefanikiwa kuwapatia vifaa vya uchimbaji madini kwa wanawake 150 wanaojishughulisha na uchimbaji madini.

Author

7 Comments

  1. Can I simply say what a aid to seek out somebody who actually is aware of what theyre speaking about on the internet. You positively know the right way to carry an issue to mild and make it important. More people need to learn this and understand this facet of the story. I cant consider youre not more popular because you undoubtedly have the gift.

  2. I discovered your blog site on google and verify a few of your early posts. Continue to keep up the superb operate. I simply further up your RSS feed to my MSN Information Reader. Searching for forward to studying extra from you afterward!…

  3. The root of your writing whilst sounding agreeable initially, did not really sit perfectly with me personally after some time. Somewhere within the paragraphs you managed to make me a believer unfortunately only for a while. I nevertheless have a problem with your jumps in assumptions and you would do nicely to fill in all those breaks. In the event you can accomplish that, I would definitely be amazed.

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Hutakiwi kuweka ‘’Lamination’’Hati miliki za Ardhi-Sanga

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya

Apartheid Victims Sue SA Gov’t R167 Million Over Lack Of Justice

The largest constitutional damages lawsuit in the country’s history has