Dark
Light

Rushwa kwa WaandIshi wa habari sababu hawalipwi vizuri-Utouh

Mkurugenzi wa Taasisi ya Wajibu Ludovick Utouh amesema katika tukio la sauti za waandishi kuwa “ ni ngumu kukomesha rushwa kwa waandishi wa habari kwa sababu hawalipwi vizuri”leo Februari 16 jijini Dar es Salaam.
February 17, 2024
by

Mkurugenzi wa Taasisi ya Wajibu Ludovick Utouh amesema katika tukio la sauti za waandishi kuwa “ ni ngumu kukomesha rushwa kwa waandishi wa habari kwa sababu hawalipwi vizuri”leo Februari 16 jijini Dar es Salaam.

“Baadhi ya vyombo vya habari vina hali ngumu ya kiuchumi ili kumuwezesha muandishi kwenda sehemu ya tukio ambapo ni mbali na eneo lake kwa lengo la kutimiza wajibu wake, lakini endapo atachukua pesa hiyo kama sehemu ya ulaghai wa kuandika mazuri ya aliyemtuma basi hiyo itakuwa rushwa.”Amesema Utouh

Mkurugenzi huyo alitoa maoni hayo baada ya swali kutoka kwa mdau Benedict Mrema kuuliza “je kuna ubaya muandishi wa habari kupewa pesa ya kwenda kufata habari mbali na eneo lake kama sehemu ya kumuwezesha kufanya kazi kwa usahihi?”

Pia Fausta Msokwa amesema muandishi wa habari kupewa bahasha ni tatizo kwa namna yoyote ile kwasabubu itamfanya aegemee upande mmoja ili siku nyingine asikose kuwezeshwa wakati wa utoaji taarifa.

Author

Leave a Reply

Your email address will not be published.

Don't Miss

Dar es Salaam Moves to End Chronic Water Shortages

Authorities in Tanzania’s bustling commercial hub are ramping up efforts

Trump Issues Warning To Iran Over Nuclear And Protests

 United States President Donald Trump has delivered a strong warning